Habari kutoka Disemba, 2009
Wapiga picha wa Kiafrika, waandishi na wasanii wapata sauti zao kwenye blogu
Kadri Waafrika wengi wanavyozidi kugundua nguvu ya kublogu kama zana ya kutoa maoni kwa kiwango cha dunia nzima, tarakimu ya wanablogu imeongezeka na pia maudhui yanayopewa kipaumbele. Kwa tarakimu hiyo ya kukua kwa blogu, wasanii wengi wa Kiafrika wamejiunga, na ongezeko kubwa likionekana kwenye blogu za mashairi kama ilivyo kwa upigaji picha unaochipukia na blogu za sanaa za maonyesho. Tunazipitia baadhi.
Israel: Kublogu Kwa Ajili Ya Mazingira Nchini Jordan
“Wanamazingira na Waandishi kutoka Palestina, Jordan na Israel watakutana huko Madaba, Jordan mwezi huu kwa ajili ya warsha ya siku 2: “Kublogu kwa Ajili ya Mazingira” tarehe 20-21 Desemba,” anaandika Muisrael Green Prophet, kwenye Mideast Youth.
Poland: Blogu Zataka Malipo
Wasomaji wa blogu zinayoongoza za lugha ya Kipolish ni lazima wameshangazwa kuona kivinjari skrini mpya ya ukaribisho kwenye moja ya tovuti zinazopendwa: Imetangaza kwamba, kuanzia Disemba 14, 2009, kupatikana kwa blogu hiyo hakuta kuwa bila ya gharama. Jakub Gornicki anaandika kuhusu habari hiyo.
Barbados, Trinidad & Tobago:Plastiki na Uchafuzi wa Mazingira
“Fanya matembezi kwenye pwani yoyote nchini Barbados – na utaona uchafu wa plastiki uliosukumwa ufukweni”: Barbados Free Press anauliza kama uuzaji wa chupa za plastiki za maji uwekewe vikwazo, wakati Mtrinidadi Keith Francis pia anaguswa na suala la uchafuzi wa mazingira kwa plastiki ulimwenguni.
Tunisia: Mwanafunzi Atupwa Gerezani kwa Kuhojiwa na Chombo cha Habari
Wanaharakati nchini Tunisia wamezindua ukurasa wa Facebook na blogu ili kumuunga mkono Mohamed Soudani, 24, aliyetoweka mnamo tarehe 22 Oktoba 2009 nchini humo mara baada ya kufanya mahojiano na Redio Monte Carlo International na vilevile Redio France International. Tangia hapo marafiki walipata fununu kwamba alikamatwa na kutupwa korokoroni na kuteswa vibaya.
Iran: Maandano ya Siku ya Mwanafunzi kwenye YouTube
Maelfu ya waandamanaji hawakuujali utawala wa Kiislamu leo kwa kuandamana wakati wa siku ya mwanafunzi, wakiimba kaulimbiu dhidi ya Ali Khamenei, kiongozi wa Jamuhuri ya Kiislamu, na wakipinga sera ya mambo ya nje ya serikali.
Brazil: Wito wa Kugomea Gazeti Linaloongoza Nchini
Wanablogu wa Brazili wamekuwa wakihamasisha mgomo dhidi ya kile walichokiita Coupist Press Party, yaani Sherehe ya Chombo cha Habari ya Kutaka Kupindua Serikali, kwa hiyo wamekuwa wakiwataka watu kuacha kununua, kusoma au kutoa maoni na badala yake kufuta usajili wao kutoka kwenye gazeti la Folha de São Paulo na tovuti yake.
Zimbabwe: Uchumi Unapinda Kona Nzuri?
Je, uchumi wa Zimbabwe unapiga kona kuelekea sehemu nzuri? anauliza mwanablogu wa Ghana, Abi.
Ghana: Rais Atta Mills Dhidi ya Chama Chake Mwenyewe?
Katika miezi michache kuelekea uchaguzi wa Rais Hohn Evans Atta Mills, wa-Ghana wengi, pamoja na wale walio nje ya nchi, waliohofu kwamba ushindi wa chama cha New Democratic Congress (NDC) ungeweza kugeuka kuwa utawala mwingine wa mwanzilishi wa chama hicho na mtawala wa zamani wa kijeshi, Rais Jerry John Rawlings.
Ghana: Fikra Juu ya Mkosi Unaoyanyemelea Mafuta
Fikra Juu ya Mkosi Unaoyanyemelea Mafuta: “kwa dibaji, Ninasema kuwa ninaamini katika haki za mali (ardhi na majengo), serikali yenye mipaka pamoja na mipango huru, japokuwa ni lazima niseme kuwa si rahisi kuidhibiti mikataba ya mafuta, hasa pale haki za mali (ardhi na majengo) zinapohusika.”