20 Disemba 2009

Habari kutoka 20 Disemba 2009

Morocco: Mwanablogu Mwingine Atupwa Gerezani

Mnamo tarehe 14 Desemba, siku ya Jumatatu, mwanablogu Bashir Hazzam na mmiliki wa mgahawa wa Intaneti Abdullah Boukhou walihukumiwa kifungo cha miezi minne jela kwa huyo wa kwanza na mwaka mmoja kwa huyo wa pili pamoja na kulipa faini ya MAD 500 (sawa na dola za Marekani 63) kila mmoja katika mahakama ya Goulmim.

20 Disemba 2009

Misri: Makao Makuu ya Kuzimu Duniani

Wanablogu na wanaharakati wengi wa Kimisri wamekuwa wakikamatwa na Usalama wa Taifa katika nyakati tafauti kwa sababu mbalimbali –za kweli au za bandia –Wa7da Masreya aliwahoji wanablogu mbalimbali na kuweka makala ya kina kuhusu mbinu za utesaji na hila za kisaikolojia ambazo wanablogu wale wamekuwa wakikumbana nazo kwenye makao makuu ya Usalama wa Taifa katika wilaya ya Jiji la Nasr.

20 Disemba 2009

Urusi: Simulizi Tatu za Umaskini Uliokithiri

RuNet Echo

Mwandishi wa habari mpiga picha wa Urusi, Oleg Klimov, anatusimulia visa vitatu vya umaskini uliokithiri ambavyo alipata kusikia habari zake wakati akisubiri treni katika kituo cha treni cha Syzran, jiji lililo katika eneo la Samara la Urusi.

20 Disemba 2009

Wapiga picha wa Kiafrika, waandishi na wasanii wapata sauti zao kwenye blogu

Kadri Waafrika wengi wanavyozidi kugundua nguvu ya kublogu kama zana ya kutoa maoni kwa kiwango cha dunia nzima, tarakimu ya wanablogu imeongezeka na pia maudhui yanayopewa kipaumbele. Kwa tarakimu hiyo ya kukua kwa blogu, wasanii wengi wa Kiafrika wamejiunga, na ongezeko kubwa likionekana kwenye blogu za mashairi kama ilivyo kwa upigaji picha unaochipukia na blogu za sanaa za maonyesho. Tunazipitia baadhi.

20 Disemba 2009