Kukamatwa, kupigwa na kuachiwa huru kulikofuata kwa wanablogu Yoaní Sánchez, Claudia Cadelo na Orlando Luis Pardo kulikofanywa na majeshi ya usalama ya Cuba tarehe 6 Novemba, kunapata matangazo mengi katika vyombo vikubwa vya habari [1] na katika ulimwwengu wa blogu pamoja na ule wa Twita. Yoani ameandika [2] (es) kuhusu tukio hilo kwenye blogu yake, Generación Y, na blogu za Kiingereza kama vile Babalú Blog [3], Repeating Islands [4] pamoja na Uncommon Sense [5] zinafuatilia habari hiyo. Mahojiano ya sauti [6] (es) na Sanches kuhusu tukio hilo yamepandishwa kwenye YouTube.
Cuba: Ukweli wa Sanchez Kutiwa Mbaroni Waibuka
· Imeandikwa na Georgia Popplewell Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza
Mada za Habari: Amerika Kusini, Cuba, Habari za Hivi Punde, Haki za Binadamu, Harakati za Mtandaoni, Uhuru wa Kujieleza