26 Februari 2009

Habari kutoka 26 Februari 2009

Clinton Azuru Indonesia

Pamoja na kukutana na viongozi wa Indonesia, Katibu wa Mambo ya Nje wa Marekani, Hillary Clinton alipata muda wa kutembelea makazi ya watu masikini mjini Jakarta. Kadhalika alitokea kwenye kipindi cha televisheni cha vijana. Ni nini maoni ya wanablogu?

26 Februari 2009

Misri: Wanablogu Wafuatilia Milipuko ya Mabomu Mjini Kairo

Mtalii wa Kifaransa ameuwawa na watu wapatao 20 wamejeruhiwa wakati bomu lilipolipuka nje ya msikiti wa Al Hussein uliopo katika eneo la utalii la Khan Al Khalili mjini Kairo. Na wakati dunia ilipokuwa inaanza kufahamu ni kipi kilichokuwa kinatokea, wanablogu wa Misri waliingia kazini haraka, wakipashana habari za yanayotukia, taarifa, uchambuzi na hofu zao.

26 Februari 2009

Martinique: Uhuru na “Ubeberu” wa Kifaransa

Wakati harakati za wafanyakazi zinaendelea huko Martinique na Guadeloupe, wanablogu wa Martinique wanapima uhuru wa Idara za Ng'ambo utamaanisha nini. Le blog de [moi] anaona dhana ya kuwa Martinique haiwezi kujitegemea ni dhana inayotusi na ya kibeberu. Wasomaji wake wanadhani kuwa ukweli wa kisiwa chochote kidogo ni kuwa kila siku kitakuwa katika kivuli cha wengine.

26 Februari 2009

Guadeloupe: Hali Tete Yazua Ghasia

Baada ya wiki za maandamano ya amani katika Idara za Ng'ambo za Ufaransa za Guadeloupe na Martinique, mambo yaligeuka na kuwa ghasia siku ya jumatatu, polisi na waandamanaji walipambana katika jiji kubwa la Guadeloupe, Pointe-a-Pitre. Wafanyakazi wanapinga ukosefu wa ajira unaoongezeka pamoja na kupanda kwa bei za bidhaa muhimu, ambazo nyingi zake huagizwa kutoka Ufaransa.

26 Februari 2009